Urusi yashambulia miundo mbinu ya Ukraine
17 Machi 2026
Matangazo
Ukraine imesema shambulio la Urusi limesababisha uharibifu wa kiwanda, bandari na miundo mbinu ya nishati katika mkoa wa Odesa usiku wa kuamkia leo.
Ukraine imefahamisha kwamba mashambulizi hayo pia yamesababisha kukatika kwa umeme kwenye baadhi ya maeneo ya makaazi Kusini kwa mkoa huo. Zelenskiy akosoa uamuzi wa kuilegezea Urusi vikwazo
Kwa mujibu wa Gavana wa Odesa Ole Kiper, kupitia ujumbe alioutowa kwenye mtandao wa Telegram, moto uliosababishwa na mashambulio hayo ulidhibitiwa haraka na kwamba hakuna aliyejeruhiwa.
Urusi pia imeshambulia bandari kubwa ya Ukraine iliyoko kwenye eneo la mto Danube
karibu na Romania ambayo ni mwanachama wa jumuiya ya NATO.
Wizara ya ulinzi ya Romania imesema inachunguza kuhusu tukio hilo.