1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Urusi yaushambulia tena mji wa Kharkiv

23 Septemba 2024

Urusi imefanya mashambulizi mapya kwenye mji wa Kharkiv nchini Ukraine usiku wa kuamkia leo, ambapo majengo kadhaa yamebomolewa na watu wapatao 20 kujeruhiwa.

Wafanyakazi wa zimamoto katika mji wa Kharkiv.
Wafanyakazi wa zimamoto katika mji wa Kharkiv.Picha: Andrii Marienko/AP Photo/picture alliance

Kwa mujibu wa gavana wa mkoa huo, Oleh Syniehubov, majengo 18 yenye ghorofa baina ya 9 na16 yameharibiwa kwa mashambulizi  hayo.

Wakaazi kadhaa wa majengo hayo wamelazimika kuhamishiwa maeneo mengine.

Kharkiv ndio mkoa wa pili kwa ukubwa nchini Ukraine, ambao umekuwa ukishambuliwa mara kwa mara tangu Urusi ilipoanza uvamizi wake mwaka 2022.

Soma zaidi: Zelensky atia saini sheria ya ongezeko la pesa kwa jeshi

Mashambulizi haya yanajiri wakati Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine akiwa ziarani nchini Marekani kuomba silaha zaidi za kukabiliana na Urusi.

Akiandika kupitia mtandao wa X, Zelensky amelaani mashambulizi hayo mapya mjini Kharkiv, akiwatolea wito washirika wake wa Magharibi kutuma silaha zaiid kuisaidia Ukraine kuwalinda raia na mali zao. 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW