1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Urusi yazidisha mashambulizi katika miji ya Ukraine

2 Machi 2022

Uvamizi wa Urusi dhidi ya Ukraine umeendelea kwa siku ya saba tangu uvamizi huo kuanza katika baadhi ya miji muhimu.

Ukraine | Gebäudebrand nach mutmasslichem Angriff auf Charkiw
Picha: Ukraine Emergency Ministry press service/AFP

Mashambulizi yameendelea katika mji wa pili kwa ukubwa wa Ukraine Kharkiv, huku hofu ikitanda huenda mashambulizi zaidi yakaulenga mji mkuu, Kyiv.

Ukraine yashutumu mashambulizi ya Urusi kama kampeni ya wazi ya ugaidi

Kufuatia mashambulizi ya ndege kwa muda wa saa 24 zilizopita hadi mapema leo, maafisa wa Ukraine wamesema watu 21 wameuawa na kituo kimoja cha polisi kimeharibiwa.

Shinikizo laongezeka dhidi ya India ilaani uvamizi wa Urusi

Watu 2,000 wameuawa Ukraine tangu uvamizi ulipoanza

Shirika la kitaifa la Ukraine linalotoa huduma za dharura limesema takriban watu 2,000 wameuawa tangu Urusi ilipoivamia Ukraine wiki iliyopita.

Kwenye ukurasa wake wa Facebook, shirika hilo limesema maafisa 10 wa kutoa huduma za dharura ni miongoni mwa waliouawa.

Urusi imesema imeendeleza mashambulizi katika miji muhimu Ukraine huku ikilenga mji mkuu Kyiv.Picha: AP Photo/picture alliance

Urusi imesema imechukua udhibiti kamili wa mji wa bandari Kherson ulioko katika bahari nyeusi. Lakini meya wa mji huo amepinga kauli hiyo akisema wangali imara ndani ya Ukraine.

Mtoto wa Museveni azusha mjadala kwa kuiunga mkono Urusi

Hata hivyo maafisa wa pande zote, Ukraine na Urusi wamesema wanajeshi wa Urusi wameingia katika mji wa pili wa Ukraine Kharkiv. Jeshi la Ukraine limeeleza kwamba mapigano yamekuwa yakiendelea katika mitaa ya mji huo wa Kharkiv.

Urusi yaongeza mashambulizi katika miji muhimu

Kufuatia mashambulizi, mashirika ya kutoa huduma za dharura yameripoti kwamba watu wanne wameuawa na tisa wamejeruhiwa mjini Kharkiv.

Urusi imeimarisha mashambulizi yake katika miji ya Ukraine ikiwemo magharibi na kusini mwa Kyiv.

Waangalizi wanaofuatilia yanayojiri kuhusiana na mzozo huo wameelezea hofu ya uwezekano wa mji mkuu Kyiv kuwa katika hatari ya kushambuliwa Zaidi kufuatia vikosi vya Urusi nje ya mji huo.

Hayo yakijiri, Uhispania ndiyo nchi ya hivi karibuni zaidi kutangaza kuipa Ukraine zana za kivita.

Maafa ya vita

Tangu uvamizi huo kuanza, Ukraine imedai kwamba wanajeshi 5,840 wameuawa. Hata hivyo takwimu hiyo haijaweza kuhakikiwa. Urusi kwa upande wake imekiri kukumbwa na maafa ila haijaweka wazi takwimu kamili.

Kulingana na wizara ya Ulinzi ya Urusi, wanajeshi wake waliharibu zana za kivita 1,500 za Ukrain zikiwemo ndege 58, drones 46 na vifaru 472.

Ukraine imekana kupata hasara hiyo kufikia sasa.

Kufuatia mashambulizi mjini Kharkiv, mashirika ya kutoa huduma za dharura yameripoti kwamba watu wanne wameuawa na tisa wamejeruhiwa.Picha: Sergey Bobok/AFP/Getty Images

Katika shambulizi la jana Jumanne lililofanywa na Urusi dhidi ya mnara wa kituo cha televisheni cha Kyiv, watu watano waliuawa. Hayo yamesemwa na Ukraine.

Hayo yakijiri naibu waziri mkuu wa Ukraine Iryna Vereshchuk ametoa wito kwa kiongozi mkuu wa kanisa katoliki Papa Francis kuzungumza na rais wa Urusi Vladimir Putin ili afungue njia kuwezesha misaada ya kiutu kupitishwa kupelekewa wahanga wa machafuko.

Kulingana na Umoja wa Mataifa takriban watu 836,000 wameyakimbia machafuko hayo kwenda nchi jirani.

(AFPE; RTRE)

 

Ruka sehemu inayofuata Gundua zaidi