1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Utafiti: kupungua kwa misaada kutasababisha vifo milioni 22

18 Novemba 2025

Zaidi ya watu milioni 22, wengi wao watoto, wako hatarini kufa kutokana na magonjwa yanayoweza kuzuilika ifikapo 2030 kwa sababu ya kupunguzwa kwa misaada ya Marekani na Ulaya.

Somalia Mogadishu 2025 | Watoto waliokimbia makazi yao ndani ya kambi ya wakimbizi ya Maslah
Watoto waliokimbia makazi yao ndani ya kambi ya wakimbizi ya Maslah nchini Somalia 05.02.2025Picha: Farah Abdi Warsameh/AP Photo/picture alliance

Zaidi ya watu milioni 22, wengi wao wakiwa watoto, wanaweza kufa kutokana na magonjwa yanayoweza kuzuilika ifikapo mwaka 2030 kwa sababu ya kupunguzwa kwa misaadana Marekani na nchi za Ulaya, kwa mujibu wa utafiti mpya. Matokeo haya ni nyongeza ya  utafiti wa awali ulioangazia misaada ya Marekani pekee na kusema kuwa kupunguzwa kwa kiwango kikubwa na Rais Donald Trump kungeweza kusababisha vifo vya ziada vya watu milioni 14.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW