Baadhi ya jamii za Tanzania zinaamini kuwa utamaduni wa kula pamoja kwenye sahani au sinia moja, unawafundisha watoto upendo na nidhamu wakati wa kula. Si kula pekee bali watu wote huketi kwenye jamvi au mkeka mmoja wanapokula. Je hali ni vipi kuhusu utamaduni huo, katika kipindi hiki cha janga la corona? Salma Mkalibala anasimulia