1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Utekaji nyara wamalizika Algeria

22 Januari 2013

Vikosi vya jeshi la Algeria vimevamia eneo la kisima cha gesi asilia jana jumamosi(19.01.2013) ili kufikisha mwisho mzozo uliosababisha vifo vya raia wa kigeni 23 na Waalgeria,saba na pia watekaji nyara wameuwawa.

epa03545840 Filipino overseas workers, who were sent home by their employer in Algeria but clarified that they were hundreds of kilometers away from a gas plant hostage crisis, arrive at the Manila international airport in Manila, Philippines 20 January 2013. Algeria's minister of telecommunications said on 20 January that he expected more bodies to be found, a day after the army launched a bloody assault on a remote gas plant where militants had held hundreds of workers captive. Algerian authorities had said that 23 captives and 32 terrorists had been killed in the In Amenas gas facility in the Sahara desert, after the military launched a final assault to end the four-day hostage standoff. EPA/ROLEX DELA PENA
Hawa ni mateka walioachwa huru AlgeriaPicha: picture-alliance/dpa

Mateka  21 wameuwawa  wakati  eneo  hilo  lilipokuwa  limezingirwa , hali  iliyotokana   na  watu  wenye  silaha  wenye  mafungamano na  kundi  la  al-Qaeda  waliposhambulia  kituo  cha  kukusanyia  gesi asilia  cha  In Amenas  ndani  ya   eneo  la  jangwa  la  sahara mapema  alfajiri  siku  ya  Jumatano, imesema  wizara  ya  mambo ya  ndani.

Wateka  nyara  32 pia  wameuwawa, na  kikosi  maalum  cha  jeshi la  Algeria  kilifanikiwa  kuwaacha  huru  wafanyakazi  685  raia  wa Algeria  pamoja  na  wafanyakazi  kutoka  nchi  za  nje  wapatao 107, taarifa  hiyo  imesema.

Mateka waliosalimika nchini AlgeriaPicha: AP

Raia wa  kigeni wauwawa

Miongoni  mwa  wale  waliouwawa  kuna  idadi  ambayo  haijulikani ya  raia  wa  kigeni , ikiwa  ni  pamoja  na  wanaotoka  Uingereza, Ufaransa, Romania  na  Marekani, na  wengi  bado  hawajulikani waliko.

Kampuni  ya  uhasindisi  kutoka  Japan  ya  JGC Corp. imesema  leo kuwa  Wajapani  10  na  wafanyakazi  wengine  saba  wa  kigeni bado  hawajulikani  waliko, lakini  imethibitisha  kuwa  wafanyakazi 61  miongoni  mwa  78 wako  salama.

Helikopta ya jeshi ikiwa angani AlgeriaPicha: Reuters

Wateka  nyara  wakiongozwa  na  Mokhtar Belmokhtar  raia  wa Algeria , ambaye  ni  kamanda  wa  zamani  wa   kundi  la  al-Qaeda katika  eneo  la  Afrika  ya  kaskazini , wamewauwa  watu  wawili katika  basi, Muingereza  na  raia  wa  Algeria , kabla  ya kuwakamata  mamia  ya  wafanyakazi  mateka wakati walipokishambulia  kituo  hicho  cha  gesi  asilia.

Kundi  la  Belmokhtar  la "Signatories  in Blood", waliotia  saini  kwa damu  limekuwa  likidai  kumalizwa  kwa  uingiliaji  kati  kijeshi  wa Ufaransa   dhidi  ya  wapiganaji  wa  Kiislamu  katika  nchi  jirani  ya Mali.

Kiongozi  huyo  wa  kundi  hilo  la  wapiganaji  ameonya  katika matamshi  aliyotoa  na  kutangazwa  jana  jumamosi  kuwa  ataripua kituo  hicho  cha  kusafisha  gesi  iwapo  jeshi  litafika  karibu  na kituo  hicho.

Katika  matamshi  yake  yaliyotangazwa  na  shirika  la  habari  la Mauritania,kamanda  wa   kikosi  cha   Al-Mulathameen , Abdul Rahman  al-Nigeri  kutoka  Niger  amesema  siku  ya  Alhamis wakati  jeshi  la  Algeria  lilipozingira  maeneo  ya  wapiganaji  wake.

Mwanajeshi wa AlgeriaPicha: Reuters

Nigeri  anasemekana  kuwa  kiongozi  wa  ngazi  ya  juu kwa kiongozi  mkuu  wa  wateka  nyara  Belmokhtar. Katika   shambulio la  Jumamosi , jeshi  la  Algeria  liliwakamata  magaidi  11, na  kundi hilo  la  kigaidi  liliuwa  mateka  wao  saba  raia  wa  kigeni.

Mauzo ya  nje  hayakuathirika

Wakati  huo  huo  Algeria  haijapunguza  mauzo  yake  ya  nje  ya gesi  baada  ya  kuanza  kwa  mzozo  huo  wa  utekaji  nyara, wizara ya  nishati  ya  nchi  hiyo  imesema.

Kituo cha gesi kilichotekwa na wapiganaji AlgeriaPicha: picture alliance / dpa

"Washirika  wetu  hawajaathirika  kutokana  na  hali  hiyo. Hatukupunguza  mauzo  yetu  ya  nje  ya  gesi, tumeweza  tu kujaliza upungufu  huo  kwa  uzalishaji  kutoka  katika  maeneo  mengine  ya nchi, " shirika  la  habari  la  APS  limemnukuu Youcef Yousfi.

Mwandishi : Sekione  Kitojo / afpe
Mhariri : Stumai George

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW