1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaNepal

Utulivu warejea Nepal

11 Septemba 2025

Hali ya utulivu inaripotiwa kurejea nchini Nepal, siku chache baada ya waandamanaji kuiporomosha serikali na kuyachoma moto majengo ya umma, likiwemo bunge.

Nepal Kathmandu | maandamano ya umma
Vijana wa Nepal wakishangiria ushindi juu ya jengo la serikali, Singha Durbar, kufuatia kuiangusha serikali ya nchi hiyo kwa maandamano ya umma.Picha: Niranjan Shrestha/AP Photo/picture alliance

Wawakilishi wa waandamanaji wanafanya mazungumzo na viongozi wa jeshi kwenye makao makuu ya jeshi mjini Kathmandu kwa lengo la kumpata kiongozi wa mpito.

Baadhi ya waandamanaji wanampendekeza jaji mkuu wa zamani, Sushila Karki, kuchukuwa nafasi hiyo.

Karki ndiye mwanamke pekee kuwahi kushikilia wadhifa wa jaji mkuu kwenye taifa hilo la Asia.

Uamuzi wa serikali kutumia vyombo vya usalama  vilivyowauwa watu 19  kuzuwia maandamano ya Jumatatu yaliyoitishwa na vijana kupinga amri ya kupiga marufuku mitandao ya kijamii, ulizusha hasira kubwa ya umma.

Maelfu ya raia walijitokeza mitaani kuishinikiza serikali na kupelekea  Waziri Mkuu Khadga Prasad Oli  kujiuzulu na kukimbia.

Hatima ya alipo Oli haijafahamika hadi sasa.

Wizara ya Afya ya Nepal ilisema idadi ya watu waliopoteza maisha kwenye maandamano hayo imefikia 25. 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW