1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUturuki

Uturuki inaamua kati ya Erdogan au Kiliçdaroglu

28 Mei 2023

Vituo vya kupigia kura vimefunguliwa asubuhi ya leo kote nchini Uturuki kwa duru ya pili ya uchaguzi wa rais itakayoamua mwanasiasa atayeliongoza kwa miaka mitano, taifa hilo la pili kwa idadi kubwa ya watu barani Ulaya.

Uchaguzi wa rais nchini Uturuki
Uchaguzi wa rais nchini Uturuki Picha: Ed Ram/Getty Images

Karibu wapiga kura milioni 61 wanashiriki uchaguzi huo unaofanyika kuanzia saa mbili asubuhi hadi majira ya saa kumi na moja jioni kwa saa za Uturuki.

Uchaguzi wa leo unafanyika baada ya duru ya kwanza kushindwa kutoa mshindi wa wazi kati ya rais aliye madarakani anayewania muhula mwingine Recep Tayyip Erdogan dhidi ya mpinzani wake mkuu Kemal Kiliçdaroglu.

Kura ya leo inatajwa kuwa kipimo cha utawala wa miongo miwili ya Erdogan anayetuhumiwa na upinzani kwa sera za "mabavu".

Uchaguzi huo unafanyika ikiwa imepita miezi mitatu tangu kutokea tetemeko kubwa la ardhi nchini Uturuki lililowaua maelfu ya watu na katikati ya mdodoro mkubwa wa kiuchumi kuwahi kushuhudiwa nchini humo.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW