1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Uturuki inapanga kurefusha mpango wa usafirishaji nafaka

5 Machi 2023

Waziri wa mambo ya nje wa Uturuki Mevlut Cavusoglu amesema nchi yake inafanya juhudi kurefusha mpango unaoungwa mkono na UN, ulioiwezesha Ukraine kusafirisha nafaka kutoka bandari zake zilizozingirwa na Urusi

Mevlut Cavusoglu in Ankara
Picha: Murat Gok /AA/picture alliance

Mpango huo wa kusafirisha nafaka kupitia bahari nyeusi uliosimamiwa na Umoja wa Mataifa pamoja na Uturuki, uliokubaliwa mwezi Julai mwaka uliopita, uliruhusu nafaka hizo kusafirshwa kutoka  bandari tatu kubwa za Ukraine.

Mpango huo ulirefushwa mwezi Novemba na sasa muda wake unakaribia kumalizika tarehe 18 mwezi Machi. 

Umoja wa Ulaya watangaza makubaliano ya kuistaki Urusi kwa uhalifu wa kivita

Waziri Cavusoglu amesema amezungumza na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kuhusu juhudi za kurefushwa kwa mpango huo.

Wiki iliyopita Urusi ilisema itakubali hilo ikiwa maslahi ya watengenezaji wake wa bidhaa za kilimo yatazingatiwa.
 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW