1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

VALETTA: Wakimbizi wa Kiafrika wapotea baharini

31 Julai 2006

Wakimbizi 17 waliotaka kuingia Ulaya kwa njia isiyo halali hawajulikani waliko baada ya boti yao kuzama nje ya pwani ya Malta.Miongoni mwo,walikuwepo watoto 8 na mtoto mchanga mmoja. Nahodha wa uvuvi wa Kitaliana aliehusika katika juhudi ya uokozi,alipozungumza na redio ya Malta alisema,alipokuwa katika boti yake nje ya mwambao wa Malta,aliwaona wakimbizi hao wakiogelea baharini.Wanaume 8 na wanawake 5 waliokolewa na wamesema wanatokea Somalia.Siku moja kabla ya hapo,wakimbizi wengine 13 wa Ki-Afrika,kutoka kundi la watu 27,walifariki baharini walipojaribu kwenda Italia.Wakimbizi hao walitokea Libya.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW