1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaVenezuela

Venezuela: Marekani imeanza kuziachia fedha ilizozizuia

28 Januari 2026

Rais wa mpito wa Venezuela Delcy Rodriguez amesema Marekani imeanza kuziachia fedha za Venezuela zilizozuiwa chini ya vikwazo vya kiuchumi vilivyowekwa na Washington wakati utawala wa Rais Nicolas Maduro.

Venezuela Caracas 2026 | Rais wa mpito, Delcy Rodriguez
Rais wa mpito wa Venezuela, Delcy Rodriguez.Picha: Federico Parra/AFP

Rodriguez ambaye alichukua hatamu za uongozi wa nchi hiyo baada ya makomandoo wa Marekani kumkamata na kumwondoa madarakani Maduro mnamo Januari 03,  ametoa taarifa hiyo kupitia hotuba kwa taifa jana Jumanne.

Serikali ya Venezuela imekuwa chini ya vikwazo vya kiuchumi vya Marekani ikiwemo marufuku ya kuuza mafuta tangu mwaka 2019 baada ya Washington kuutilia mashaka ushindi wa Maduro kwenye uchaguzi wa mwaka 2018.

Wakati wa awamu ya kwanza ya utawala wa Rais Donald Trump, Marekani ilizuia pia fedha za Venezuela zilizowekwa kwenye akaunti za kimataifa ambazo serikali mjini Caracas ilikadiria kuwa thamani yake inafikia dola bilioni 30.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW