1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Vienna. Shirika la Atomic halifahamu iwapo Iran inataka bomu la kinuklia.

5 Machi 2007

Kiongozi mkuu wa shirika la umoja wa mataifa la nishati ya Atomic , Mohammed El Baradei, amesema kuwa shirika lake bado haliwezi kutathmini iwapo Iran inataka kuwa na silaha za kinuklia.

Katika mkutano wa bodi ya magavana wa shirika hilo la IAEA mjini Vienna , El Baradei amesema kuwa baada ya uchunguzi wa muda wa miaka minne , shirika hilo limefikia hali ya mkwamo.

Ameongeza kuwa anaimani kuwa suluhisho kuhusiana na suala la kinyuklia la Iran linaweza tu kufikiwa kupitia majadiliano.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW