1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Vifo vyaongezeka Ukraine kufuatia mashambulizi ya Urusi

29 Desemba 2023

Urusi imefanya mashambulizi makubwa nchini Ukraine kwa kufyetua makombora 122 pamoja na ndege kadhaa zisizo na rubani. Hadi sasa raia wapatao 24 wamearifiwa kuuawa huku wengine kadhaa wakijeruhiwa.

Avdiivka, Ukraine | rais Volodymyr Zelenskyy akiwa na makamanda ya jeshi lake kitengo cha ardhini.
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy akipokea melezo kuhusu maendeleo ya mapigano kutoka kwa jeshi lake.Picha: Ukrainian Presidential Press Office/AP/picture alliance

Kamanda wa Jeshi la anga la Ukraine Mykola Oleshchuk ameandika kwenye ukurasa wake wa mtandao wa kijamii Telegraph kwamba lilikuwa "shambulio kubwa zaidi la anga" tangu Urusi ilipoanzisha uvamizi huo Februari mwaka jana (2022).

Balozi wa Marekani mjini Kyiv Bridget Brink amesema hii leo kuwa mashambulizi hayo ya Urusi dhidi ya Ukraine yanadhihirisha hitaji la kuipatia ufadhili Ukraine ili kuendelea kupigania uhuru wake.

Soma pia: Watu 24 wauawa Ukraine katika wimbi jipya la mashambulizi

Ikulu ya White House imekuwa ikishinikiza kupata msaada zaidi wa kijeshi kwa Ukraine licha ya upinzani mkali kutoka kwenye Baraza la Congress.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW