1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaBurundi

Vifo vya ripotiwa Bujumbura kufuatia milipuko ya Jumanne

1 Aprili 2026

Miripuko ya silaha nzito yaliutikisa mji wa Bujumbura usiku wa Jumanne, maafisa wathibitisha vifo na majeruhi huku jeshi likisema matokeo yatabaki siri.

Burundi Bujumbura 2026 | Milipuko na moshi baada ya moto katika kambi ya jeshi
Miripuko kadhaa ilisikika Jumanne usiku kwenye mji mkuu wa Burundi, Bujumbura, baada ya moto kuzuka kwenye ghala za silaha la kambi moja ya kijeshi mjini humoPicha: Ju Yinhe/Xinhua/IMAGO

Huzuni imetanda katika baadhi ya wakaazi wa mitaa mbali mbali ya jiji la Bujumbura. Taarifa zinasema silaha hizo ziloonekana mabaki yake kama mtwangiyo wa kinu zilianguka katika mitaa tafauti ya jiji.

Ikiwa île iliyo karibu na kambi ya Musaga eneo la tukio aidha mitaa ya mbali kama umbali wa kilometa 10 na eneo hilo.

Mtaani Gihosha kaskazini mwa jiji nyumbani kwa sheikh Kida silaha hiyo ilianguka uwani na kumkata mguu binti yake, huku mkewe sheikh na mfanyakazi wake wakijeruhiwa vibaya.

Si mbali na hapo kombora lilianguka nyumbani kwa baba mwengine na kumpiga kichwani na kufariki papo hapo.

"Wako waliokufa na wengine kujeruhiwa"

Msemaji wa jeshi, Gaspard Baratuza, amesema hitilafu ya umeme kwenye ghala la silaha la jeshi hilo kwenye kambi ya Musaga ndiyo sababu ya miripuko hiyoPicha: Ju Yinhe/Xinhua/IMAGO

Gavana wa mkoa wa Bujumbura Aloys Ndayikengurukiye anasema miripuko hiyo kiini chale ni moto uloripuka ndani ya ghala ya silaha katika kambi ya musaga. Na kuwataka raia kusalia watulivu na kurudi katika majukumu yao ya kila siku.

"Baada ya kuwasiliana na maafisa wa jeshi tulitaka kuwatuliza nyoyo raia kwani kumekuwa na taarifa kuwa ni shambulio lilotokea. Tuna wahakikishia kuwa ni moto uloripuka katika ghala ya silama katika kambi ya musaga. Wapo waliokufa na wengine kujeruhiwa kwa sasa tunakusanya matokeo kutoka tarafa mbalimbali", alisema  Ndayikengurukiye.

Gavana huyo wa Bujumbura amebaini pia kuwepo na pale makombora hayo yalipoangukia na kusalia bila kuripuka hivyo amewataka raia kutowa taarifa kwa watawala wa jeshi ama kwa walinda usalama, ili kuepusha kusababisha maafa mengine.

Jeshi limejizuwia kutowa taarifa na kwamba matokeo ya hasara ́yatasalia siri jeshini.

Taarifa zinasema shirika la msalaba mwekundu limejielekeza wakati huu ni kiripoti  katika jela kuu la mpimba  si mbali na eneo la tukio ambako pia makombora hayo yaripotiwa kuangukia na kusabasha pia hasara.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW