1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Vijana wa kiislamu wahujumu msikiti Burundi:

26 Novemba 2003
BUJUMBURA: Watu kadhaa wamejeruhiwa jana, vijana wa kiislamu walipofyetua risasi kwenye msikiti mmoja kaskazini-magharibi mwa Burundi, wakati watu wakisali sala ya IDI-FITR kwa ajili ya kumalizika funga ya mwezi mtukufu wa Ramadhani,- kwa mujibu wa shirika la habari la Burundi. Washambuliaji wane wametiwa nguvuni na askari polisi, na wanashikiliwa katika gereza moja la CIBITOKE kaskazini-magharibi mwa Burundi. Vijana hao ni wafuasi wa tawi lililoasi la chama cha waislamu wa Burundi, COMIBU.
Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW