1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Viongozi wa G7 kufanya mkutano wa siku tatu nchini Canada

15 Juni 2025

Viongozi wa G7 watawasili leo katika eneo la Kananaskis, Alberta nchini Canada kwa mkutano wa kilele wa siku tatu utakaoanza rasmi kesho Jumatatu.

Mawaziri wa mambo ya nje wa G7 katika picha ya pamoja wakati wa mkutano wao huko Anagni Italia mnamo Novemba 25 ,2024
Mawaziri wa mambo ya nje wa G7Picha: Claudia Greco/REUTERS

 

Mbali na mvutano huo wa Mashariki ya Kati, viongozi hao pia wanatarajiwa kuangazia vita nchini Ukraine, mizozo ya biashara ya kimataifa, uhamiaji, na kupata ufikiaji wa malighafi muhimu.

Mazungumzo ya pembezoni mwa mkutano huo pia yanatarajiwa.

Mkutano wa G7 waijadili Ukraine na uchumi wa dunia

Watakaohudhuria mkutano huo ni pamoja na Rais wa Marekani Donald Trump, Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz, Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron na waziri mkuu wa Uingereza Keir Starmer.

Waziri mkuu wa Canada Mark Carney ni mwenyeji mkutano huo, unaokuja baada ya ushindi wake katika uchaguzi, ambao kwa sehemu umetokana na msimamo wake mkali dhidi ya tishio la Trump la kuifanya Canada kuwa jimbo la 51 la Marekani.