SiasaMarekani
Mazungumzo kati ya Iran na Marekani kufanyika Roma Jumamosi
17 Aprili 2025
Matangazo
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araqchi na Kiongozi wa Qatar Sheikh Tamim bin Hamad Al-Thani wamewasili mjini Moscow ambapo wanatarajiwa kukutana na Rais wa Urusi Vladimir Putin, huku Waziri wa Ulinzi wa Saudi Arabia Mwanamfalme Khalid bin Salman akielekea mjini Tehran.
Duru ya kwanza ya mazungumzo kati ya Marekani na Iran ilifanyika mjini Muscat huko Oman, katika wakati ambapo rais Donald Trump na Kiongozi Mkuu wa Iran Ali Khamenei wamekuwa wakirushiana maneno makali na vitisho.
Hata hivyo mazungumzo hayo yanatarajiwa kuwa magumu kwa kuwa Iran imesisitiza kwamba haki yake ya kurutubisha madini ya urani haiwezi kuwa sehemu ya majadiliano.