1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUkraine

Viongozi wa magharibi waikosoa hotuba ya rais Putin

21 Februari 2023

Viongozi kadhaa wa magharibi wameikosoa hotuba ya rais Vladimir Putin wa Urusi aliyoitoa mapema leo ambapo ameahidi kuendelea na vita nchini Ukraine.

Belgien Brüssel | EU-Gipfel zu Ukraine
Picha: Olivier Matthys/AP Photo/picture alliance

Waziri Mkuu wa Italia Giorgia Meloni anayeitembelea Ukraine ameitaja hotuba hiyo ya Putin kuwa "propaganda" huku mshauri wa usalama wa taifa wa  Marekani Jake Sullivan akisema madai yaliyotolewa na rais Putin kuwa sababu ya Urusi kuingia vitani ni ya "kipuuzi".

Katika hotuba yake mbele ya bunge la taifa rais Putin alisema mataifa ya magharibi ndiyo yaliilazimisha Moscow kuingia vitani baada ya kugeuka kitisho kwa usalama wa Urusi.

Kwa upande wake mkuu wa Jumuiya ya Kujihami ya  NATO Jens Stoltenberg amesema madai hayo hayana ukweli kwa sababu rais Putin ndiye alianzisha vita ya kutaka kuishikilia mateka Ukraine na bado anaendekeza uhasama.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW