1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Viongozi wa Ulaya wapanda jukwaani Davos

20 Januari 2026

Rais wa Halmashauri Kuu ya EU, Ursula von der Leyen ameuelezea mpango wa Rais Donald Trump wa Marekani kuziwekea ushuru nchi za Ulaya kwa kupinga mpango wake wa Greenland, kama kosa hasa kati ya washirika wa muda mrefu.

Ubelgiji Brüssel 2025 | Emmanuel Macron katika mkutano wa waandishi wa habari
Rais wa Ufaransa Emmanuel MacronPicha: Stephanie Lecocq/REUTERS

Von der Leyen alikuwa akizungumza Davos nchini Uswisi kulikofunguliwa rasmi Jukwaa la Kiuchumi la Dunia, ambapo ameutilia shaka uaminifu wa Trump akisema, mwaka jana alikubali kutoziwekea ushuru zaidi nchi za Umoja wa Ulaya.

Wakati huo huo, Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amesema ulimwengu unapitia kipindi ambacho sheria za kimataifa zinapuuzwa na sheria zinazoonekana kuwa zenye umuhimu ni zile za wenye nguvu tu.

Akiwa Davos, Macron ameilaani hatua ya Marekani kutaka kuidhoofisha Ulaya kupitia makubaliano ya kibiashara ambayo yanakiuka maslahi yake ya uuzaji bidhaa nje na kulitaka bara hilo likubaliane kikamilifu na matakwa yake.

Aidha, Macron amesema hakuna mkutano wa kundi la mataifa saba yaliyoendelea kiuchumi duniani ya G7, uliopangiwa kufanyika siku ya Alhamisi.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW