1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroSudan

Vita na uporaji vyaripotiwa katikati mwa Sudan

1 Julai 2024

Wapiganaji wa kikosi cha wanamgambo wa RSF nchini Sudan wameripotiwa kupora katika makaazi ya watu, sokoni, maduka na kuteka baadhi ya hospitali katika mkoa wa Sennar jana Jumapili.

Uharibifu katika soko huko al-Fasher, mji mkuu wa jimbo la Darfur Kaskazini mwa Sudan.
Uharibifu katika soko huko al-Fasher, mji mkuu wa jimbo la Darfur Kaskazini mwa Sudan.Picha: AFP

Kwa mujibu wa makundi ya haki za binadamu na wakaazi walioshuhudia, uvamizi huo umewalazimu maelfu ya watu kukimbia.

Wanamgambo wa RSF waliokuwa ndani ya magari ya wazi wakiwa na bunduki walivamia mji wa Singa ulio kilometa 350 kusini mashariki mwa mji mkuu Khartoum.  

Soma pia: UN: Sudan yakabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula 

Mapambano hayo yaliyoanzishwa na RSF mapema wiki hii yalianza kwa kundi hilo kushambulia kijiji cha Jebal Moya kabla ya kuendelea katika eneo la Singa.

Mapema Jumamosi RSF ilidai kuteka jengo kuu la jeshi huko Singa.

Hata hivyo  msemaji wa jeshi la Sudan Brigedia Nabil Abdalla amesema kuwa jeshi lilifanikiwa kukomboa eneo hilo na kuwa mapigano yaliendelea hadi Jumapili asubuhi.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW