1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Von der Leyen kuwania ukuu wa NATO

1 Aprili 2023

Rais wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Ulaya, Ursula von der Leyen, yuko mbioni kuwania uteuzi wa mkuu mpya wa jumuiya ya kujihami ya NATO.

EU Die Präsidentin der Europäischen Kommission Ursula von der Leyen hält eine Grudsatzrede zu den Beziehungen zwischen der EU und China
Picha: Valeria Mongelli/AFP

Haya yameripotiwa jana na gazeti la The Sun lililonukuu duru za kidiplomasia.

Ripoti ya gazeti hilo la The Sun likinukuu vyanzo vya Uingereza, imesema kuwa Uingereza huenda ikapinga kuchaguliwa kwa von der Leyen ambaye aliwahi kuhudumu kama waziri wa ulinzi wa Ujerumani na kutaja rekodi yake mbaya ya usimamizi wa jeshi la nchi hiyo.

Soma zaidi: NATO, EU zaapa uungaji mkono zaidi kwa Ukraine

Gazeti la Ujerumani la Welt am Sonntag pia limeripoti kuwa Waziri Mkuu wa Uhispania Pedro Sanchez na Waziri wa Ulinzi wa Uingereza Ben Wallace ni miongoni mwa wawaniaji wanaoongoza kumrithi mkuu wa sasa wa NATO, Jens Stoltenberg, ambaye muda wake wa uongozi unafikia kikomo mwezi Oktoba baada ya kuhudumu kwa takriban miaka tisa.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW