1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Vyama vya SPD na CDU vyaunda muungano mpya Brandenburg

16 Machi 2026

Chama cha Social Democratic Party, SPD, na chama cha kihafidhina cha Christian Democratic Union, CDU, vimesaini makubaliano ya kuunda serikali ya muungano katika jimbo la Brandenburg mashariki mwa Ujerumani.

Deutschland Potsdam 2026 | Woidke na Redmann
Vyama vya SPD na CDU vyaunda muungano mpya BrandenburgPicha: Soeren Stache/dpa/picture alliance

Makubaliano hayo yaliosainiwa na waziri mkuu wa jimbo hilo Dietmar Woidke wa SPD, pamoja na mwenyekiti wa CDU wa eneo hilo Jan Redmann katika mji mkuu wa Potsdam, karibu na Berlin, yanaweka vipaumbele vya serikali mpya kwa kipindi cha miaka mitatu na nusu ijayo.

Serikali ya awali iliyoongozwa na SPD ilivunjika mapema Januari baada ya mivutano ya ndani katika chama kipya cha BSW.

Woidke alikataa kuitisha uchaguzi wa mapema na badala yake akaunda muungano mpya na CDU, hatua inayofanana na muundo wa serikali ya kitaifa inayoongozwa na Kansela Friedrich Merz.

Chama cha BSW, kinachojulikana kwa msimamo wake kuikosoa jumuiya ya NATO, kilishindwa kuvuka kizingiti cha asilimia tano katika uchaguzi wa shirikisho mwezi Februari, ingawa kilishika nafasi ya tatu katika uchaguzi wa jimbo hilo mwaka 2024.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW