1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUfaransa

Ufaransa yajiandaa kwa mgmo mkubwa wa wafanyakazi

6 Machi 2023

Ufaransa inakabiliwa na mgomo wa nchi nzima Jumanne, uliotangazwa na vyama vya kutetea maslahi ya wafanyakazi, kupinga mpango wa Rais Emmanuel Macron wa kutaka kuongeza umri wa kustaafu, kutoka 62 mpaka 64.

Frankreich | Landesweite Streiks gegen geplante Rentenreform
Picha: Julien Mattia/Le Pictorium/MAXPPP/dpa/picture alliance

Mgomo huo ni awamu nyingine ya mapambano kati ya serikali ya mrengo wa kati na wapinzani wasiotaka mageuzi ya mfumo wa pensheni, baada ya kushuhudiwa maandamano makubwa mara tano mwaka huu.

Vyama vya wafanyakazi vimeitisha mgomo na maandamano nchi nzima, hatua ambayo Waziri wa Usafiri Clement Beaune, ametahadharisha kwamba itakuwa na athari kubwa sana kote nchini Ufaransa.

"Kutakuwa na athari kubwa sana" kutokana na mgomo huo, Waziri wa Uchukuzi Clement Beaune alisema kwenye shirika la utangazaji la kikanda la France-3 siku ya Jumapili. "Ninajua kuwa kwa watu wengi itakuwa usumbufu mkubwa."

Waziri wa Kazi Olivier Dussopt, akizungumza kwenye shirika la utangazaji la FranceInfo siku ya Jumatatu, alisema "kuonyesha kutokubaliana ni halali, lakini haipaswi kusababisha kuzuia nchi, ambayo itakuwa hatari kwa uchumi wetu."

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW