1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Waandamanaji wakamatwa Kenya wakipinga muswada wa fedha

18 Juni 2024

Zaidi ya waandamanaji 200 wamekamatwa katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi katika maandamano yanayoendelea dhidi ya mapendekezo ya ongezeko la kodi yaliyoko kwenye muswada wa fedha unaotarajiwa kuwasilishwa bungeni.

Maandamano Kenya
Polisi wakipambana na waandamanaji katika moja ya maandamano Kenya.Picha: Thomas Mukoya/REUTERS

Makundi ya Kiraia yamesema maandamano hayo na mpango wa kukaa mbele ya jengo la bunge vitaendelea licha ya waandamanaji wenzao 210 kukamatwa.

Kamanda wa Polisi wa Nairobi Admason Bungei amesema hakuna kundi lililoruhusiwa kuandamana mjini humo.

Mapema, polisi walitumia gesi ya kutoa machozi kuwatawanya mamia ya waandamanaji na kusababisha biashara kufungwa kwa muda kutokana na hofu ya uporaji.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW