1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wadephul akiri "hali tete" kwenye NATO chini ya Trump

13 Februari 2026

Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani Johann Wadephul amesema Mkutano wa Usalama wa Munich -MSC- ambao unafunguliwa rasmi hii leo, unamaanisha fursa ya kuangazia upya ushirikiano miongoni mwa washirika wa Jumuiya ya NATO.

Belgien Casteau 2004 | Sherehe ya NATO kuadhimisha wanachama saba wapya kujiunga na jumuiya hiyo ya kijeshi
Hamasa imeendelea kutolewa kwa bara la Ulaya kuangazia namna ya kurekebisha uhusiano miongoni mwa mataifa wanachama wa Jumuiya ya NATOPicha: Yves Boucau/dpa/picture alliance

Akizungumza na kituo cha utangazaji cha Ujerumani, ARD mapema leo, Wadephul amekiri mivutano iliyoshuhudiwa katika siku za karibuni inaufanya ushirika huo wa kijeshi kuwa chini ya shinikizo kubwa.

Uhusiano baina ya Marekani na washirika wa NATO yameingia dosari tangu Rais Donald Trump aliporejea madarakani mwaka uliopita.

Trump pamoja na baadhi ya maafisa waandamizi wa serikali yake wamekuwa wakiwakosoa vikali washirika wao wa Ulaya kwa kile ambacho Washington imesema ni kushindwa kuchangia vya kutosha kwenye bajeti ya ulinzi na kulitegemea zaidi jeshi la Marekani.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio anaiwakilisha nchi yake kwenye mkutano huo, unaohudhuriwa pia na viongozi wa Ulaya na Mkuu wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Ulaya, Ursula von der Leyen.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW