Mamlaka zaifanyia upekuzi Deutsche Bank Ujerumani
28 Januari 2026
Matangazo
Msemaji wa Deutche Bank amethibitisha Jumatano kuwa upekzi huo unafanyika katika ofisi hizo na kuwa inatoa ushirikiano kamili kwa waendesha mashtaka.
Kwa mujibu wa gazeti la kila siku la Süddeutsche, ukaguzi huo unahusiana na uvunjaji wa sheria katika biashara zinazofanywa kati ya benki hiyo na makampuni yanayohusishwa na bilionea wa Urusi Roman Abramovich.
Vita vya Ukraine vyatajwa
Mfanyabiashara huyo mkubwa aliwekewa vikwazo na Umoja wa Ulaya kutokana na uvamizi wa Urusi nchini Ukrane. Gazeti hilo limesema ofisi zilizopekuliwa ni za Berlin na katika makao makuu ya benki hiyo mjini Frankfurt.