1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wafugaji wataka Tanzania izuiwe kutumia ardhi

25 Januari 2022

Wafugaji wa jamii ya Maasai waliopo katika wilaya ya Ngorongoro mkoani Arusha wataka Tanzania izuiwe kutumia radhi iliyotengwa kulinda mazalia ya wanyamapori.

Maasai aus Loliondo in Tansania
Picha: Judith Fehrenbacher

Wafugaji  wa jamii ya Maasai wanaoishi katika wilaya ya Ngorongoro mkoani Arusha Tanzania, wamewasilisha pingamizi katika mahakama ya Afrika Mashariki wakitaka serikali ya Tanzania izuiwe kuitumia ardhi yenye kilometa za mraba 1500, kipindi ambapo mahakama hiyo bado haijatoa maamuzi ya kesi ya msingi.   

Mwaka 2013, serikali ya Tanzania ilitangaza kupunguza ukubwa wa eneo la ardhi lenye kilometa za mraba 4000 hadi kufikia 1500, kwa lengo la kulinda mazalia ya wanyamapori, huku  vijiji 14  vyenye wakazi  takribani elfu sabini , vikiathirika kwa kukosa makazi na malisho ya mifugo. 

Wananchi hao wa wilaya ya Ngorongoro  mwaka 2017, walifungua kesi katika mahakama ya Afrika Mashariki wakipinga uamuzi huo wa serikali ya Tanzania kwakuwa haukua na ushirikishwaji wa wananchi, lakini kabla mahakama hiyo haijatoa uamuzi serikali imeanza kuligawa eneo hilo. 

Msajili wa Mahakama ya Afrika Mashariki Yufunalis  Okubo, amethibitisha kupokea maombi ya wafugaji hao ya kuitaka mahakama iweke zuio la kutumika kwa ardhi wakati kesi ikiendelea. 

Veronica Natalis- Arusha

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW