1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaIran

Wagombea urais wa Iran wakabiliana katika mdahalo wa mwisho

Sylvia Mwehozi
3 Julai 2024

Wagombea wawili wa urais wa Iran hapo jana walikabiliana katika mdahalo wa pili na wa mwisho wa Televisheni kabla ya duru ya pili ya uchaguzi utakofanyika siku ya Ijumaa.

Iran I Präsidentschaftwahl - Kandidatendebatte im TV
Mdahalo wa wagombea wa urais nchini IranPicha: irna

Wagombea hao walijadili athari za vikwazo vya kiuchumi vilivyowekwa na Marekani na mataifa mengine ya Magharibi na kuwasilisha mipango yao kuhusu kufufua mkataba wa nyuklia na mataifa yenye nguvu duniani.

Mdahalo huo uliwakutanisha mwanamageuzi asiyejulikana sana Masoud Pezeshkian na mpatanishi wa zamani wa masuala ya nyuklia mwenye msimamo mkali Saeed Jalili.

Soma pia: Raia wa Iran wanapiga kura leo kumchagua rais mpya 

Iran itafanya duru ya pili ya uchaguzi wa rais Ijumaa, ikiwa ni mara ya pili tangu Mapinduzi ya Kiislamu ya  mwaka 1979.

Ni asilimia 39.9 pekee ya wananchi waliojitokeza kushiriki duru ya kwanza ya uchaguzi wiki iliyopita.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW