Wahamiaji 50 wa Sudan waaga dunia Libya
17 Septemba 2025
Matangazo
Shirika la Uhamiaji la Umoja wa Mataifa, IOM, limesema siku ya Jumatano.
Manusura 24 wameokolewa na kuliambia shirika hilo kuwa kulikuwa na karibu watu 75 katika boti hiyo, wote wakiwa wametokea Sudan.
Chanzo cha moto huo na kituo ilipoanzia safari hiyo na kituo ilikokuwa inaelekea bado havijulikani kwa sasa.
"Hatua ya haraka inahitajika ili kusitisha majanga ya aina hiyo baharini," lilisema shirika la IOM katika taarifa.
Kulingana na takwimu za IOM, karibu watu 1,225 wamefariki dunia wakati wakijaribu kuvuka bahari ya Mediterenia mwaka huu pekee.
Idadi kamili ya waliofariki lakini inatarajiwa kuwa juu zaidi kwa kuwa boti nyingi ambazo hazijasajiliwa hufanya safari zake usiku na haibainiki zinapozama.