Wahamiaji 53 hawajulikani walipo baada ya meli kuzama Libya
9 Februari 2026
Matangazo
Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia masuala a uhamiaji IOM Jumatatu limesema watu 53 wamekufa au hawajulikani walipo baada ya meli kuzama katika bahari ya Mediterania karibu na pwani ya Libya.
Shirika hilo limesema katika taarifa yake kuwa meli hiyo ilipinduka kaskazini mwa Zuwara, Libya, mnamo Februari 6 na ni wanawake wawili pekee wa Nigeria waliookolewa wakati wa operesheni ya utafutaji na uokoaji iliyofanywa na mamlaka za Libya.
IOM imeongeza kwamba mmoja wa manusura alisema alipoteza mumewe na mwingine akasema alipoteza watoto wake wawili katika mkasa huo.