1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JangaLibya

Wahamiaji 61 wapoteza maisha baharini njiani kwenda Ulaya

17 Desemba 2023

Wahamiaji 61 ikiwemo wanawake na watoto wamekufa baada ya boti waliyokuwa wakiitumia kuvuka bahari ya Mediterrenia kupata ajali nje kidogo ya pwani ya Libya

Moja ya boti zinazotumiwa na wahamiaji
Wahamiaji hutumia njia hatari na vyombo visivyo thabiti.Picha: DARRIN ZAMMIT LUPI/REUTERS

Taarifa hizo zimetolewa na Shirika la Uhamiaji la Umoja wa Mataifa IOM kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa X.

Ikiwanukuu manusura wa mkasa huo, IOM imesema boti hiyo iliyokuwa imewabeba watu wasiopungua 86 iling´oa nanga kwenye mji wa mwambao wa Zuwara ulio umbali wa kiasi kilometa 110 kutoka mji mkuu wa Libya, Tripoli.

Inaarifiwa kuwa mawimbi makubwa yaliipiga boti hiyo na kuwa chanzo cha ajali iliyogharimu maisha ya watu 61.

Ajali hiyo ya jana Jumamosi ndiyo mkasa wa hivi karibuni kabisa kwenye mfululizo wa masaibu yanayowakumba wahamiaji wanaotumia njia hatari kujaribu kuingia barani Ulaya.

Umoja wa Mataifa unakadiria watu 2,200 wamekufa ndani ya mwaka huu pekee kwa kuzama baharini wakiwa njiani kukimbilia nchi za Ulaya.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW