Wahamiaji tisa waliofukuzwa Marekani wawasili Cameroon
1 Mei 2026
Matangazo
David amesema wahamiaji hao waliowasili nchini humo siku ya Jumatano ni raia wa Ghana, Angola, Ethiopia na Congo-Brazzaville na walikuwa kundi la tatu la uhamishaji huo tangu Januari.
Wameungana sasa na wahamiaji wengine kumi na saba waliofukuzwa awali na Marekani hadi Cameroon.
Kwa mujibu wa gazeti la New York Times, Marekani inailipa Cameroon dola milioni 30 kuwa sehemu ya mpango huo.
Nchi nyingine za Afrika zilizofikia makubaliano kama hayo ni Equatorial Guinea, Ghana, Rwanda, Sudan Kusini, Eswatini na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.