1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wahamiaji wapatao 50 kutoka Sudan wafariki baharini Libyahi

17 Septemba 2025

Wahamiaji wapatao 50 kutoka Sudan wamekufa baada ya boti yao kushika moto katika pwani ya Libya siku ya Jumapili. Haya yamesemwa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Wahamiaji, IOM.

Boti  ya walinzi wa pwani ya Italia wakivuta mabaki ya boti ya wahamiaji haramu mnamo Septemba 15, 2002
Boti ya walinzi wa pwani ya Italia Picha: picture-alliance/dpa

Manusura 24 waliookolewa, wamewaambia maafisa wa shirika hilo kuwa takriban watu 75 walikuwa ndani ya boti hiyo, wote kutoka Sudan.

Baada ya kushauriana na mamlaka nchini Libya, msemaji wa IOM amesema chanzo cha moto huo bado hakijabainika pamoja na mahali boti hiyo lilipotokea ama kukusudiwa kuelekea.

Katika taarifa, IOM imesema hatua za haraka zinahitajika kumaliza majanga hayo baharini.

Kulingana na takwimu za IOM, kufikia sasa katika kipindi cha mwaka huu, takriban watu 1,225 wamekufa wakijaribu kuvuka bahari ya Mediterania, ingawa idadi kamili inaaminika kuwa ya juu zaidi kwa sababu boti nyingi ambazo hazijasajiliwa hufanya safari za usiku na kukosa kutambuliwa zinapozama.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW