Wairani washiriki Ijumaa ya kwanza tangu kuanza kwa vita
6 Machi 2026
Matangazo
Mikanda ya video iliyochapishwa mtandaoni imeonesha makundi makubwa ya wanaume na wanawake waliovaa nguo nyeusi wakiwa wamekusanya kwa sala ya Ijumaa kwenye msikiti mkuu wa Imam Khomeini katikati mwa mji mkuu, Tehran.
Ulinzi ulikuwa umeimarishwa wakati wa ibada hiyo ambayo pia ni ya kwanza tangu Marekani na Israel zilipomuua Kiongozi Mkuu wa Iran Ayatolah Ali Khamenei.
Kwenye miji mingine ikiwemo Borujerd na Zahedan umati wa watu wenye bendera za nchi hiyo ulisongamana kuelekea misikitini chini ya kiwingu cha mashambulizi ya anga yanayoendelea.