Wajerumani miongoni mwa waliofariki kwa ajali ya ndege Kenya
28 Oktoba 2025
Matangazo
Ripoti zinaarifu kuwa ndege hiyo ilikuwa njiani kuelekea katika mbuga ya kitaifa ya wanyama ya Maasai Mara.
Kulingana na taarifa ya shirika la ndege hiyo Mombasa Air Safari, ndege hiyo ilikuwa imewabeba raia wawili wa Ujerumani, wanane kutoka Hungary pamoja na rubani mmoja raia wa Kenya.
Mamlaka zinasema ndege hiyo imeanguka katika eneo lenye milima na misitu lililoko karibu kilomita 40 kutoka uwanja mdogo wa ndege wa Diani.
Mamlaka zinachunguza chanzo cha kuanguka kwa ndege hiyo ingawa inaripotiwa kuwa kulikuwa na mvua kubwa katika eneo la pwani ya Kenya wakati ndege hiyo ilipoanza safari yake.