1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wajerumani wanapiga kura leo

22 Septemba 2013

Wajerumani wanapiga kura leo(22.09.2013) wakati kansela wa sasa Angela Merkel akionekana kuwa atashinda kipindi cha tatu cha uongozi, lakini huenda akalazimika kuunda serikali na mahasimu wake wakuu.

Bildnummer: 60485186 Datum: 14.09.2013 Copyright: imago/Caro Vioel, Schleswig-Holstein, Deutschland - Wahlkampf zur Bundestagswahl am 22.09.2013. Auf einem Feld in Nordfriesland stehen Grossplakate der Spitzenkandidaten von CDU und SPD. Peer Steinbrueck wirbt mit dem Slogan -Das Wir entscheidet-. Angela Merkel mit -Kanzlerin fuer Deutschland-. (QF, europäisch, Peer Steinbrück, Persönlichkeiten, Steinbrück, Viöl, wählen) 0HX130914D800CARO.JPG MODELxRELEASE:xNO, PROPERTY RELEASE: NO PUBLICATIONxNOTxINxPOL x0x xkg 2013 quer 2013 Angela Merkel Aufschrift aussen Aussenaufnahme Bundeskanzlerin Bundespolitik Bundestag Bundestagswahl Bundestagswahl 2013 Bundestagswahlkampf CDU deutsch Deutschland Europa europaeisch Grossplakat Grossplakate Kampagne Kandidat Kandidaten Kanzlerkandidat Kanzlerkandidaten Marketing Merkel Nordfriesland Partei Parteien Peer Steinbrueck Persoenlichkeiten Plakat Plakate Plakatwerbung Politik Politiker Politikerin politisch Poster Schleswig-Holstein Schrift Schriftzug Slogan Slogans SPD Spitzenkandidat Spitzenkandidaten Steinbrueck Vioel waehlen Wahl Wahlen Wahlkampf Wahlkampfwerbung Wahlplakat Wahlplakate Wahlslogan Wahlspruch Werbeplakat Werbung Westeuropa 60485186 Date 14 09 2013 Copyright Imago Caro Schleswig Holstein Germany Election campaign to Federal election at 22 09 2013 on a Field in North Friesland Stand Large posters the Leading candidates from CDU and SPD Peer Steinbrueck advertises with the Slogan the We decides Angela Merkel with Chancellor for Germany QF Euro Peer Steinbrück Personalities Steinbrück choose JPG Property Release No PUBLICATIONxNOTxINxPOL x0x xkg 2013 horizontal 2013 Angela Merkel Inscription exterior Outside view Chancellor Federal politics Bundestag Federal election Federal election 2013 Bundestag election campaign CDU German Germany Europe Eisch Europe Large poster Large posters Campaign Candidate Candidates Chancellor candidate Chancellor candidate Marketing Merkel North Friesland Party Parties Peer Steinbrueck Personalities Billboard Posters Poster advertising politics Politicians Politician politically Poster Schleswig Holstein Font emblem Slogan Slogans SPD Top candidate Leading candidates Steinbrueck choose Choice Choose Election campaign Election campaign advertising Election billboard Election posters Election slogan Slogan Billboard Advertising Western Europe
Angela Merkel(kulia) na Peer Steinbrück (kushoto)Picha: imago stock&people

Baada ya kuuongoza uchumi mkubwa wa kwanza katika bara la Ulaya kupita katika msukosuko mkubwa wa madeni, Merkel amejitokeza kuwa maarufu zaidi kutokana na anavyotoa uhakika kama atoavyo mama kwa mtoto wake, kwa viongozi ambao wameingia matatani kama vile nchini Ufaransa, Ugiriki, Italia na Uhispania.

Wachunguzi wa maoni ya wapiga kura wanaashiria kuwa wapiga kura watamchagua tena kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 59, ambaye jina lake la utani , ni "Mutti", yaani mama anayeonekana kushabihiana zaidi na jina analotambulishwa nalo kila mara la mwanamke mwenye nguvu duniani.

Mgombea wa chama CDU Angela MerkelPicha: Reuters

Nani atakuwamo katika serikali

Lakini suala muhimu hapa litakuwa nani ataunda serikali nae? "Ni mara chache hali imekuwa ya karibu hivyo. Muungano wa Merkel una wingi mdogo tu kwa mujibu wa maoni ya wapiga kura , limesema gazeti la Sueddeutsche Zeitung, na kuongeza kuwa wengi wa wapiga kura wapatao milioni 62 wanaamua katika dakika za mwisho nani wampigie kura.

Merkel anajigamba kuwa muungano wake wa sasa wa siasa za wastani za mrengo wa kulia umekuwa na mafanikio makubwa tangu baada ya Ujerumani mbili kuungana mwaka 1990, kwa kuwa na uchumi imara na kiwango cha ukosefu wa ajira kikiwa chini ya asilimia saba.

Mgombea wa chama cha SPD Peer SteinbrückPicha: Reuters

Lakini lengo alilojiwekea kwa ajili ya chama chake cha Christian Democratic Union (CDU) kubaki madarakani na washirika wake wadogo katika serikali, chama kinachopendelea wafanyabiashara cha Free Democratis, FDP, linategemea majaaliwa ambayo hayana hakika kwa chama hicho kidogo. "Kuendelea kutawala pamoja na washirika wake wa sasa ni suala ambalo halina uhakika," Gero Neugebauer, mtaalamu wa masuala ya siasa kutoka chuo kikuu huria cha mjini Berlin amesema.

Iwapo muungano huo utafeli kupata wingi wa kutosha kuweza kutawala, Merkel anaweza kulazimika kuingia katika mikono ya mahasimu wake wa jadi, chama cha Social Democratic , SPD, ambacho alikishirikisha katika kile kinachojulikana kama muungano mkuu, lakini usio na mapenzi, katika kipindi chake cha kwanza cha uongozi.

Chama mbadala

Huku washirika wake wa Ulaya wakikodolea macho, chama kinachopinga muungano wa Ulaya , chama chaguo mbadala kwa Ujerumani, The Alternative for Germany, (AfD) kinaweza pia kupata mafanikio, ama kwa kuvutia kura za kutosha kuingiza wabunge katika bunge la Ujerumani ama kwa kuzipoteza kura za wapiga kura wa siasa za wastani za mrengo wa kulia.

"Kwa kansela Merkel chama hicho kisichopendelea muungano wa Ulaya kinakuwa tatizo," limesema gazeti la Spiegel mtandaoni katika mkesha wa uchaguzi. "Iwapo chama hicho kinachopinga kitafaulu kuvuka kizingiti cha asilimia tano na kuingia bungeni , hali hiyo inataigharimu mno muungano wa njano na nyeusi yaani vyama tawala vya sasa vya CDU,CSU na FDP," limeongeza gazeti hilo.

Mwenyekiti wa chama kidogo cha FDP-Philip Rösler (kushoto)Picha: Getty Images

Chaguzi tatu za kabla ya uchaguzi huu, zimeonesha kuwa chama cha AfD, ambacho kinataka kuachana na sarafu ya euro na kuvunjwa kwa muungano wa mataifa ya eneo la euro, kimeshindwa kuvuka kiunzi cha asilimia tano zinazotakiwa kwa chama kuingia katika bunge.

Lakini baadhi ya wadadisi na wachunguzi wa maoni ya wapiga kura hawajaondoa uwezekano wa chama hicho kufanya vizuri huku kukiwa na hofu mpya ya Ugiriki kuomba msaada mpya, na kusisitiza kuwa ni vigumu kutathmini nafasi za chama hicho kwasababu hakina rekodi maalum ya uchaguzi na waungaji wake mkono huenda wasikiunge mkono kama walivyofanya katika uchunguzi wa maoni.

Merkel kwa mara nyingine amesisitiza umuhimu wa Ulaya kwa Ujerumani katika kampeni ya dakika za mwisho kuweza kupata kura mjini Berlin jana Jumamosi (21.09.2013), akisema kuwa nchi yake " inaweza tu kufanya vizuri kwa muda mrefu iwapo Ulaya nzima itafanya vizuri".

Mkutano wa kampeni wa chama cha SPDPicha: Getty Images

"Hii ndio sababu uimarishaji wa sarafu ya euro sio tu ni mzuri kwa ajili ya Ulaya lakini pia kwa maslahi ya Ujerumani," amesema wakati bendi ya muziki ikiimba , "Angie auokoe ulimwengu". Waungaji mkono wa hatua imara za kuchochea ukuaji wa uchumi wameweka matumaini yao kwa chama cha SPD ambacho mgombea wake Peer Steinbrück , mwenye umri wa miaka 66, amekuwa akihangaika kupata kitu kinachoweza kuwavuta wapiga kura na bado yuko nyuma ya Merkel katika maoni ya wapiga kura kwa alama 13.

Waziri wa zamani wa fedha katika uongozi wa Merkel mwaka 2005-2009 katika ule muungano mkuu, Steinbrück amejiingiza katika matatizo wakati wa kampeni hii, hivi karibuni kabisa akionesha kidole cha kati kikiashiria matusi katika picha iliyochapishwa katika kurasa za mbele za magazeti, ikiwa ni jibu la kimya kimya kwa swali aliloulizwa kuhusiana na kuyumbayumba kwa nafasi yake ya kugombea ukansela.

Mwandishi: Sekione Kitojo / afpe / rtre

Mhariri: Bruce Amani

Ruka sehemu inayofuata Gundua zaidi
Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW