Wajumbe wa Marekani na Iran wakutana Geneva
17 Februari 2026
Wajumbe wa ngazi za Juu wa Iran na Marekani wanakutana kwa mazungumzo kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran, yanayosimamiwa na Oman mjini Geneva.
Mazungumzo hayo yatakayoendeshwa bila ya kuwakutanisha moja kwa moja wajumbe hao yanafanyika katika ubalozi wa Oman mjini Geneva.
Tehran imeonesha kuwa tayari kupunguza shughuli za mradi wake wa nyuklia, ikitaka badala yake kuondolewa vikwazo vikali vya kiuchumi.Iran na Marekani kuendeleza mazungumzo Uswisi
Hata hivyo Jamhuri hiyo ya kiislamu pia imeshasema haitokuwa tayari kujadili kuhusu suala la kupunguza idadi ya makombora yake au kuacha kuyaunga mkono makundi ya wanamgambo.
Mazungumzo ya Geneva yanakuja katikati ya mivutano ya wiki kadhaa kati ya mataifa hayo mawili baada ya rais Donald Trump kutishia kuishambulia Tehran kufuatia hatua ya kuuwawa kwa waandamanaji wanaoipinga serikali ya Iran.