Wajumbe wa Marekani wako Israel kwa mazungumzo na Netanyahu
24 Januari 2026
Matangazo
Msemaji wa ofisi ya waziri mkuu wa Israel amethibitisha kuwa mkutano huo ulipangwa lakini hakutoa maelezo zaidi.
Wakati huo huo, Wizara ya Afya ya Palestina huko Gaza imesema kuwa shambulizi la Israel limewaua watu watatu, wakiwemo watoto wawili katika matukio mawili tofauti kaskazini mwa Ukanda wa Gaza.
Taarifa kutoka kwa jeshi la Israel imesema wanajeshi wake wanaofanya operesheni katika eneo la kaskazini mwa ukanda huo waligundua kwamba wanamgambo kadhaa walivuka na kuingia eneo lisiloruhusiwa wakatega kifaa cha kilipuzi katika eneo hilo, na kuwasogelea maafisa hao hali iliyowasababishia hatari.