Wakatoliki wasubiri kuchaguliwa kwa Papa mpya
7 Mei 2025
Misa hiyo inaongozwa na mkuu wa Chuo cha Makadinali, Giovanno Battista Re, kama ibada ya mwisho hadharani kabla ya makadinali hao kushiriki mkutano wa faragha wa kumchagua mrithi wa Papa Francis.
Soma pia: Baraza Maalumu la kumchagua Papa kuanza leo Vatican
Watajifungia kwenye kanisa hilo kwa muda usiojulikana hadi pale mmoja miongoni mwao atakapofanikiwa kupata theluthi mbili ya kura na kutawazwa rasmi kuwa kiongozi mkuu wa kanisa hilo lenye waumini wapatao bilioni 1.4 ulimwenguni kote.
Waumini na wafuatiliaji wengine kote duniani watasubiri ishara ya kuchaguliwa kwa papa mpya kupitia moshi utakaotoka kwenye chimni iliyofungwa juu ya Kanisa la Sistine.
Soma pia: Makadinali wawili kukosa kongamano la kumchagua papa mpya
Moshi mweupe utakapofuka itakuwa ni ishara kuwa baraza hilo la makadinali limefanikiwa kumchagua kiongozi mpya wa kanisa.