1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wakenya waendelea kuomboleza kifo cha Raila Odinga

15 Oktoba 2025

Taifa la Kenya linaendelea kuomboleza kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Raila Amollo Odinga, aliyefariki dunia leo huko Kerala nchini India akiwa na umri wa miaka 80.

Nairobi 2016 | Marehemu Raila Odinga enzi za uhai wake
Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Kenya Raila Amollo Odinga, alifariki dunia Jumatano 15.10.2025 huko Kerala nchini India Picha: Kevin Midigo/AFP

 Polisi wa India wamesema Odinga amefariki kutokana na mshtuko wa moyo. Mamia ya watu wamekusanyika kutoa heshima zao katika makazi ya Odinga jijini Nairobi, huku Rais William Ruto akitangaza siku saba za maombolezo na kuandaa mazishi ya kitaifa akimtaja  Odinga  kama mwanasiasa hodari wa Kenya:

" Ninatangaza kipindi cha siku saba za maombolezo ya kitaifa ambapo bendera zitapepea nusu mlingoti katika Jamhuri ya Kenya na katika balozi zetu zote nje ya nchi, ni ishara ya heshima kwake. Nimeahirisha shughuli zangu zote za umma kwa siku zijazo, na ninawaomba pia viongozi na watumishi wengine wote wa umma kufanya vivyo hivyo," alisema Rais Ruto.

Viongozi mbalimbali wa dunia kuanzia Afrika, Asia na kwengineko wametuma salamu zao za rambirambi kufuatia kifo cha kiongozi huyo ambaye ameiacha alama isiyofutika katika siasa za  Kenya.

 

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW