1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wakimbizi wa DRC wakimbilia Rwanda

25 Oktoba 2022

Maelfu ya wakaazi wa mashariki mwa Kongo wanaendelea kuyahama makaazi yao, kuepuka mapigano mapya yaliyozuka hivi karibuni baina ya jeshi la serikali na waasi wa M23. Mwandishi wa DW katika eneo hilo.

DR Kongo Flüchtlinge
Picha: AFP via Getty Images

Katika tangazo lake mbele ya vyombo vya habari  mjini Goma,msemji wa jeshi jenerali sylvain Ekengeameeleza kua bado mapigano makali yanaendelea katika baadhi ya vijiji  wilayani Rutshuru ikiwemo Ntamugenga ambamo alilituhumu  kundi la M23 kuwauwa raia zaidi ya watatu na kuwajeruhi wengine kadhaa kwa risasi.

Wakati huo huo, hali ilikuwa ya wasiwasi jana (Jumatatu) kutwa katika mji mdogo wa Rubare kwenye barabara inayo elekea Goma ambamo wananchi walilazimika kuanza kufunga maduka na wengine kukimbia  baada yakuanguka kwa bomu  ndani ya bwawa la kufugia samaki nje kidogo na mji huo. katika mahojiano maalumu na idhaa hii , meja Willy Ngoma  msemaji wa kundi la waasi wa M23  ambaye amekiri pia ongezeko la vifo vya raia tangu kuzuka kwa mapigano hayo amekuwa na haya yakujulisha.

Kwa sasa  karibu eneo lote linalo  dhibitiwa na waasi ikiwemo Ntamugenga limebaki bila wakaazi  ambao baadhi  wamekimbilia katika maeneo yanayo dhaniwa kuwa tulivu.

Soma zaidi:Tshisekedi aiandama Rwanda Umoja wa Mataifa

Hata hivyo, kulingana na ripoti ya ofisi ya umoja wa mataifa yakuratibu masuala ya kibinadamu, OCHA,  wakimbizi zaidi ya elfu 20  wamelikimbia wimbi hili jipya la mapigano katika wilaya ya Rutshuru huku zaidi ya wengine 2500 wakiuvuka mpaka kuelekea katika nchi jirani ya Uganda tangu kuzuka kwa mapigano hayo.

DW: DRC

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW