1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wakristo kote ulimwenguni waadhimisha Ijumaa Kuu

11 Aprili 2023

Kiongozi Mkuu wa Kanisa Katoliki Duniani Papa Francis ataungana na waumini wa kikristo ulimwenguni kote kwa ajili ya ibada ya Ijumaa Kuu ambayo ni kumbukumbu ya mateso na kifo cha Yesu Kristo.

Indien Christen
Picha: Avishek Das/ZUMA Press Wire/picture alliance

Papa Francis ataongoza ibada ya Ijumaa Kuu katika Kanisa la Mtakatifu Petro mjini Vatican, baada ya kuwaongoza waumini katika kufuata njia ya Msalaba.

Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani Papa FrancisPicha: Evandro Inetti/ZUMA Press Wire/picture alliance

Ijumaa Kuu ni sehemu ya Wiki Takatifu, inayoanza siku ya Jumapili ya Matawi hadi Jumapili ya Pasaka ambapo kulingana na imani ya Wakristo, husherehekea kufufuka kwa Yesu Kristo.

Papa Francis mnamo siku ya Jumamosi iliyopita aliruhusiwa kutoka hospitali moja ya mjini Rome alikokuwa amelazwa kwa ajil ya kutibiwa matatizo ya kifua. Taarifa ya makao makuu ya kanisa katoliki mjini Vatican ilisema wakati huo kwamba Baba Mtakatifu atatekeleza ratiba kamili ya Wiki Takatifu, pamoja na ibada ya Ijumaa Kuu pamoja na kushiriki kwenye Misa ya Jumapili katika Uwanja wa Kanisa la Mtakatifu Petro.

Waumini wa Kikristo wakiadhimisha siku ya Ijumaa Kuu mjini Addis Ababa, Ethiopia.Picha: Seyoum Getu/DW

Mapema jana Alhamisi, Papa Francis aliongoza Misa katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro kama sehemu ya miadi yake katika Wiki Takatifu.

Hapa nchini Ujerumani kumekuwepo utamaduni wa watoto kuandika barua na kuelezea hisia zao kupitia kwenye kijiji cha Ostereistedt kilichopo kaskazini mwa Ujerumani. Kwa mujibu wa shirika la Posta wakati huu wa kuadhimisha Ijumaa Kuu barua zipatazo alfu 70 kutoka kwa watoto zimepokelewa.

Mpokeaji barua za Pasaka za watoto "Easter Bunny"Picha: Focke Strangmann/dpa/picture alliance

Mpokeaji barua hizo "Easter Bunny" amesema watoto kutoka sehemu mbalimbali wanataka amani duniani wengine wametaka Chokoleti na hata tiketi za kuingia sinema na mengine mengi. Utamaduni wa kupokea barua za Watoto wakati wa pasaka katika mji wa Ostereistedt ulianza miaka 40 iliyopita.

Chanzo: DPA

 

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW