1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wanaharakati waandamana viwanja vya ndege Ujerumani

13 Julai 2023

Wanaharakati wa mazingira wa kundi linaloitwa Letzte Generation au Kizazi cha Mwisho nchini Ujerumani wamefanya maandamano kwa muda wa saa mbili katika viwanja vya ndege vya Dusseldorf na Hamburg siku ya Alhamis.

Aktion Letzte Generation am Flughafen Hamburg
Picha: Bodo Marks/dpa/picture alliance

Maandamnao hayo yalitatiza usafiri wakati ambapo msimu wa likizo ndefu katika majira ya joto unaendelea.

Msemaji wa polisi amesema shughuli za ndege zilisimamishwa katika uwanja wa Hamburg tangu saa 12:00 asubuhi baada ya watu tisa kuingia katika eneo la uwanja wa ndege bila idhini na kujilaza kwenye barabara ya kurukia ndege.

Hivi sasa polisi wanajaribu kuwaondoa watu hao kutoka kwenye eneo hilo.

Safari za ndege kadhaa kwenye uwanja wa Hamburg zimefutwa.

Soma zaidi: Polisi Ujerumani wawahamisha wanaharakati kupisha mgodi wa makaa

Katika uwanja wa ndege wa Dusseldorf ulio magharibi mwa Ujerumani, safari zimeanza tena baada ya watu saba kuingia uwanjani bila idhini na kujilaza kwenye barabara ya kurukia ndege.

Waandamanji wa kundi la Letzte Generation mara kwa mara huzuia magari barabarani na kutatiza shughuli kwenye viwanja vya ndege nchini Ujerumani.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW