Wanajeshi wanane wa Marekani wauwawa
10 Novemba 2007Matangazo
Wanajeshi hao walikuwa wakirudi kwenye mkutano na viongozi wa kijiji jana alasiri katika jimbo la Nuristan wakati wanamgambo walipowashambulia kwa maroketi na risasi.
Imeelezwa kwamba walishambuliwa kutoka sehemu kadhaa za maadui kwa wakati mmoja na kwamba wanajeshi wengine wanane wa Marekani na 11 wa Afghanistan wamejeruhiwa.
Kuuwawa kwa wanajeshi hao sita wa kunafanya jumla ya wanajeshi wa Marekani waliouwawa nchini Afghanistan kufikia 100 mwaka huu na kuufanya mwaka huu kuwa wa maafa makubwa kabisa kwa Marekani tokea kuvamiwa kwa nchi hiyo na mwaka 2001.