Wanajeshi wawili wa kitaliana wamepotea Afghanistan
23 Septemba 2007Matangazo
Roma:
Wanajeshi wawili wa kitaliana wanaotumikia kikosi cha kimataifa cha kulinda amani nchini Afghanistan hawajulikani waliko.Wizara ya mambo ya nchi za nje ya Italy imesema mjini Roma ,mawasiliano yamevunjika pamoja na wanajeshi hao.Haijulikani lakini kama wametekwa nyara au la.