1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Migogoro

RSF wakubali kusitisha vita ili kuruhusu misaada Sudan

6 Novemba 2025

Wanamgambo wa kundi la RSF la nchini Sudan wamesema wameuridhia mpango wa usuluhishi ulioratibiwa na Marekani wa kusitisha vita ili kupisha msaada wa kiutu.

Majeruhi waliokimbia mapigano El Fasher wakipatiwa matibabu katika hospitali ya muda iliyo chini ya shirika la madaktari wasio na mipaka 03.11.2025
Wakaazi wa El Fasher wanakabiliwa na hali mbaya ya kiutuPicha: Mohamed Jamal/REUTERS

Hatua hiyo imefikiwa wakati picha mpya za Satelaiti zimebaini ishara za uwepo wa makaburi ya halaiki katika mji wa El Fasher nchini Sudan kulingana na ripoti ya watafiti wa Chuo Kikuu cha Yale iliyotolewa leo Alhamisi.

Ushahidi wa mauaji ya nyumba kwa nyumba wabainishwa

Ripoti hiyo imetolewa wiki moja baada ya ripoti za mauaji ya kimbari katika eneo hilo. Tangu wakati huo, picha za Satelaiti zimebainisha ushahidi wa mauaji ya nyumba kwa nyumba, makaburi ya watu wengi, maeneo yaliyojaa damu na miili inayoonekana ardhini.

Kutokana na kuzuiliwa kwa mawasiliano, na kutokufikika kwa urahisi, picha za satelaiti zinasalia kuwa moja ya njia chache za kuufuatilia mzozo unaoendelea kwenye maeneo yaliyopewa kisogo ya Sudan ukiwemo mji wa El Fasher.