1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Migogoro

Wanamgambo wanaoiunga mkono serikali ya Kongo waingia Uvira

18 Januari 2026

Wanamgambo wanaoiunga mkono serikali ya Kinshasa wanaofahamika kwa jina "Wazalendo" wameingia katika mji wa kimkakati wa Uvira baada hivi karibuni ya waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda kutangaza kuondoka mjini humo.

Uvira, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, 2025
Waasi wa M23 walipokuwa wakikagua silaha zilizosalimishwa na wanamgambo wanaoiunga serikali ya Kongo 15.12.2025Picha: Daniel Buuma/Getty Images

Vyanzo vya ndani viliripoti Jumamosi kuwa viliwashuhudia wapiganaji wa M23 wakiondoka Uvira. Kisha, Jumapili, wanamgambo wanaoiunga mkono serikali waliingia katika maeneo ya kusini mwa Uvira.

Wanajeshi wa Kongo wanatarajiwa kuingia Uvira hivi karibuni

Gavana wa Mkoa wa Kivu Kusini Jean Jacques Purusi amethibitisha kuwa wanamgambo hao wameingia Uvira na kuwa wanajeshi wa Kongo watafuata. Zaidi kupitia taarifa yake kwa vyombo vya habari Purusi amesema wapiganaji wa M23 wako katika milima ya Uvira wakiwa wameelekeza silaha zao kwenye mji huo na maeneo yanayouzunguka. Ameongeza pia kuwa baadhi ya waasi hao wamesalia Uvira.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW