SiasaBenin
Wanamgambo wauwa wanajeshi 15 Benin
6 Machi 2026
Matangazo
Wanamgambo hao wajiitao Kundi la Kuusaidia Uislamu na Waislamu (JNIM) limesema liliivamia kambi hiyo ya Kofouno karibu na mpaka wa Niger siku ya Jumatano.
Jeshi la Benin lilithibitisha vifo hivyo hapo jana. Msemaji wa jeshi, Kanali James Johnson, ameliambia shirika la habari la AFP kwamba mashambulizi hayo yamewajeruhi pia wanajeshi wengine watano.
Afrika ya Magharibi imekuwa ikikabiliwa na ongezeko la mashambulizi ya makundi yenye siasa kali, hasa nchini Burkina Faso, Mali na Niger, lakini katika miaka ya karibuni, mashambulizi hayo yameenea hadi Benin na Togo.