1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Migogoro

Wanamgambo wenye mafungamano na IS waua watu 15-DRC

3 Januari 2026

Wanamgambo wanaohusishwa na kundi linalojiita Dola la Kiislamu IS, wamefanya mashambulizi ya wakati mmoja katika vijiji vitatu mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Oicha 2025 | Askari wakiwa kwenye doria baada ya mashambulizi ya waasi wa ADF
Askari wakiwa kwenye doria baada ya mashambulizi ya waasi wa ADF 2025Picha: Shi Yu/Xinhua/picture alliance

Wanamgambo wanaohusishwa na kundi linalojiita Dola la Kiislamu IS, wamefanya mashambulizi ya wakati mmoja katika vijiji vitatu mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, na kuwaua watu zaidi ya 10. Taarifa hizo ni kwa mujibu wa vyanzo vya kijeshi na kiraia.

Mashambulizi hayo yanadaiwa kufanywa na wanamgambo wa kundi la ADF huko kaskazini magharibi mwa jimbo la Kivu Kaskazini.

Kwa mujibu wa kiongozi mmoja wa eneo hilo Macaire Sivikunula, vijiji vyote vitatu vilishambuliwa kwa wakati mmoja na wanamgambo wa ADF. Mashambulizi hayo yalisababisha wanakijiji kuingiwa na hofu huku milio ya risasi ikisikika kati ya saa 8:00 usiku hadi saa 10:00 usiku. Watu 15 waliuawa na nyumba 13 kuchomwa moto. Jeshi la Kongo limesema askari wake wawili pia wameuawa.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW