1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wanaoiunga mkono Ukraine wataka msaada usisitishwe

16 Aprili 2026

Nchi zinazoiunga mkono Ukraine zimesisitiza tena dhamira yao ya kuendelea kuiunga mkono kijeshi nchi hiyo katika mkutano uliofanyika mjini Berlin.

Katibu Mkuu wa NATO Mark Rutte
Katibu Mkuu wa NATO Mark RuttePicha: Anna Rose Layden/REUTERS

Akizungumza baada ya mkutano huo, Katibu Mkuuwa Jumuiya ya Kujihami ya NATO Mark Rutte amesema, licha ya changamoto zinazoikabili Ulaya, ni sharti wahakikishe kuwa wanaweza kuisaidia Ukraine kikamilifu.

Waziri wa ulinzi wa Ujerumani Boris Pistorius kwa upande wake amesema msaada kwa Ukraine haustahili kupunguzwa kivyovyote vile licha ya macho yote ya dunia kuelekea katika mzozo wa Mashariki ya Kati.

Kundi la ulinzi kwa Ukraine ni kundi la takriban mataifa 50 yanayoisaidia Ukraine na msaada wa kijeshi.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW